Mafunzo 7 yaliyomo katika kitabu cha why "A" students work for "C" students and "B"students work for the government



Kila mmoja kwa nafasi yake angependa kujifunza zaidi kuhusiana na fedha, wapo wengi ambao hushindwa kutambua ni wapi elimu hii wanaweza kuipata, na wachache hufanikiwa kuipata katika umri tofauti tofauti wapo wale ambao hufanikiwa wakiwa na umri mdogo yaani kutokana na mazingira waliyokuzwa nayo na wapo wale ambao huipata elimu hiii tayari wakisha kuwa wakubwa kiasi cha kujitambua. Hakika zipo makala mbalimbali ambazo zinazungumzia masuala ya uchumi ama fedha kwa ujumla, pia vitabu ambavyo huandikwa na watu mashuhuri kama vile Robert Kiyosaki, Brian Tracy pia Wallace D Wattles na wengineo wengi

Lakini leo nimekuletea makala ambayo inazungumzia  masuala ya upatikanaji wa fedha kupitia uwezo wetu wa akili na jinsi vile tunaweza kuwaza sisi wenyewe Makala hii inazungumzia mambo saba ambayo yamekuwa mafunzo yanayotoa elimu ya fedha na kuwasaidia watu engi mno katika dunia yetu. Kitabu hiki kimeandikwa na Robert Kiyosaki na kinaitwa   "why "A" students work for "C" students and "B"students work for the government" 

       kukipata kitabu hiki kwa mfumo wa pdf bure bofya link hii hapa chini


Utakapopakua kitabu hiki utaweza kujifunza mambo mengi sana kuhusu fedha na njia zake za kuimanage hata isikupotee tena pale uipatapo, na yafuatayo ni mafunzo 7 ambayo tunayapata ndani ya kitabu hiki

1.     kila mtu ni "Genius"

Robert Kiyosaki amekuwa na sababu kubwa sana ya kusema kwamba katika hii dunia kila mtu ni "Genius" sababu hizi amezitaja katika sehemu mbalimbali ya kitabu hiki, mwanzo tu alianza kwa kusema kauli ya Albert Einstein uliosema
    
          "But if you judge the ability of a fish to climb a tree, it will live its whole                                                                 life believing that it is stupid"

Kwa mantiki hii watu wengi huangahika mfano wa samaki anyetamani kupanda mti, huku wa wenyewe wakijizani ni wapumbavu kwa kushindwa kufaulu kwa kila kitu ambacho wanakihitaji, lakini hakika wengi wao huwa si kosa lao.....
                                      
                                      "go to school to get a good job"
muda mwingine huwa wazazi wetu hutuambia maneno haya ambayo huonesha moja kwa moja kuwa tunaenda kusoma hili tuajiriwe na kupata pesa tu tofauti na dunia ya leo, Robert asema zaidi kwamba kwanini somo la pesa halikufundishwa mashuleni endapo kama wote tunaenda shule hili tupate kazi ambayo itatulipa pesa?
 watu wengi huenda shule sehemu ambayo haifundishi san kuhusiana na kipaji ama "genius" ya mtu mmoja mmoja na hivyo hupoteza uwezo wao 

2.  Elimu ni kuhusiana na "content" and "Context"

Elimu ya kitaaluma ni elimu ambayo imejikita katika content au "maudhui" tu  mfano, ukienda shule unatakiwa ujue kuhusiana na kusoma, kuandika, mahesabu  pasipo na kujali kuwa wewe mwenyewe ni lazima uhusishwe katika mambo haya hapa mtu ambaye yeye amejaaliwa katika mwili mfano, watu wa riadha na michezo tofauti hakika hawatoweza kuongoza katika masomo haya ya darasani
"Context" ni mwanafunzi mwenyewe ambaye shule na elimu inayotoa huwa haimuangalii nini mwanafunzi huuyu anahitaji 
 mfano wapo wanaoenda shule huku wakiamini kuwa watakuja kuwa wafanyabiashara wakubwa sana duniani lakini mwisho wa siku huangukia na kuwa madaktari sehemu ambayo hawakuwahi kuwaza kama wangekuwa huko

3.  Shule haziwaandai wanafunzi kwa ajili ya kukabiliana na dunia ya halisi

kila mtoto ni "Genius" lakini kwa bahati mbaya  kipaji chake ama uwezo alionao hauwezi kutambulika kupitia shule zetu ambazo kila siku hufundisha kitu sawa kwa wanafunzi wote ambao wna ndoto tofauti tofauti na kwa hali hii hakika huwezi gundua ni nini ama nani utakuwa hapo mbele, niw achache tu mabao hufanikiwa na wengi wao huishia kuwa tu viongozi wa makampuni fulani makampuni ambayo wamiliki ni wale mabao hawajamaliza shule au hawakwenda kabisa shule!!!

Shule huwafanya wanafunzi wawe washindanaji amabpo hushindania kupata A darasani na si kuwa wapambanaji au watengenezaji wa ajira katika dunia halisi

4. Elimu ya Uchumi huanza tangu utoto

Jambo hili ndilo ambalo limemfanya Robert aandike kitabu hiki huku akiwashauri wazazi kuhusiana na maisha ya kifedha kwa ajili ya watoto wao hapa Robert alimaanisha kuwa tunatakiwa kuwafundisha watoto wtu tangu wakiwa wadogo kuhusiana na mambo yote yanayohusiana na pesa, Endapo tutafanya hivi watoto wetu watakuwa ana uwezo mkubwa wa kukabiliana na  dunia iliyo halisi

5. Nini hugharimu mpaka kuwa Tajiri

Watu wengi huamini kuwa matajiri ni wezi.......japo wapo....
lakini jambo lililo jema kutambua ni kwamba kila mtu ananweza kuwa Tajiri kulingana na vile tu mtu atakavyojiweka na kujisumbua kuutafuta huo utajiri  watu wengi hufikia  malengo yao ya utajiri kwa kufanya kazi kwa bidii, kutengeneza biashara, kuweka budget nzuri, kutenegenza ajira zitakazokuletea faida.  Wanafunzi wengi ambao hufanikiwa katika dunia halisi ni wale ambao husoma mafunzo ambayo hayafundishwi darasani,....

              soma maelezo zaidi kutoka kitabu cha Rich dad Poor dad

6. Nguvu ya lugha 

Robert anaeleza kuwa tangua lipokuwa mdogo kila alipojifunza lugha hakuwahi kufanya vizuri katika mafunzo hayo ya lugha hila siku moja alipoudhuria katika mkutano wa baba yake ambaye ni tajiri ndipo aligundua kuwa kwa mtu kuwa tajiri si lazima ajue lugha nyingi, hila ni uwezo wake wa kutambua tu lugha ya kitaaluma mfano mtu wa sheria bhasi huwa anaongea kugha ya kisheria, mtu uhasibu huwa anaongea kugha yake ya kihasibu, hivyo nai vyema sana kujua lugha moja kwa umakini zaidi ila uijue katika taaaluma tofautitofauti hiyo itasaidia sana

7. Funzo juu ya "mali na madeni"

Robert anaeleza kuwa katika safari ya kuwa tajiri ni lazima kuweza kutambua juu ya mali na madeni kwani mali ndiye kitu ama jambo la pekee litakalokufanya uweze kuingiza pesa kwa wingi, kwa vike unavyomiliki mali nyingi ndvyo hivyo hivyo utakavyokuwa na uwezo nkubwa wa kupata pesa,,hii ni tofauti sana na mtu mabaye anakuwa na madeni mengi mno mtu huyu lazima moja kwa moja atakuwa amsikini akwani kila pesa anayopata bhasi itakuwa inaishia ttu katika kulipa madeni ambayo anadaiwa.

Shukrani sana kwa kufatilia makala hii hadi mwisho naamini umejifunza mambo mebgi kutoka hapa, tuanakuomba uzidi kuwa karibu nasi kwani bado kuna mengi yaliyo mazuri zaidi ya hili yanakuja 


Comments